Bei ya mafuta duniani imeanza kupungua tena kwa mara ya kwanza tangu mwezi Oktoba.
Sasa pipa moja linauzwa kwa chini ya dola 60.
Hata hivyo baraza la mawaziri kutoka nchi zinazouza mafuta kwa wingi OPEC limesema kupungua kwa bei kutaathiri uchumi wao.
Wamesema nchi nyingi ambazo zilitarajia mafuta kuuzwa kwa dola 70 mwaka 2019 zitahitaji kupanga upya bajeti zao.
Baadaye wiki hii mawaziri hao wanatarajiwa kukutana kujadili swala hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |