Shirika la ndege la Qatar limeanzisha safari za moja kwa moja kati ya Doha na Mombasa nchini Kenya.
Wadau wa sekta ya hoteli wamepongeza hatua hiyo ambayo itasaidia kukuza utalii.
Mkurungezi wa chama cha wenye hoteli, Sam Ikwaye amesma kuanzishwa kwa safari hizo ni dhihirisho kuwa mji wa Mombasa umeanza kuvutia biashara a utalii kimataifa.
Wikendi hii ndege ya Qatar aina ya Airbus A320,ilitua katika uwanja wa kimataifa wa Moi kwenye safari yake ya kwanza.
Qatar Airways itafanya safari nne kwa wiki, Jumanne, Alahamisi, Jumamosi na Jumapili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |