Wizara ya elimu ya Kenya na mashirika yake yamezindua mpango wa kuimarisha uandikishaji wa wasichana shuleni katika kaunti zilizoachwa nyuma, na tatizo kubwa linalowakabili wasichana hao ni kutojua kusoma na kuandika. Waziri wa elimu wa Kenya Bibi Amina Mohamed amesema mpango huo wa miaka mitano unalenga kutimiza usawa wa kijinsia katika uandikishaji shuleni kwenye kaunti zilizo pembezoni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |