Halamashauri ya kuuza nje bidhaa za kilimo nchini Rwanda NAEB imezindua mradi wa kusaidia vijana kukuza zaidi ya miti milioni 100 ya matunda kati ya sasa na mwaka 2024.
NAEB imesema mradi huo unalenga kufungua nafasi zaidi za ajira kwa vijana.
Kwenye uzinduzi wa mradi huo, zaidi ya miti 8,000 ilipandwa ikiwemo miembe, mipapai, michungwa na mingine.
Mratibu wa NAEB katika mkoa wa kusini Alex Nkurunziza amesema kati ya mwezi Juni 2017 na Julai mwaka 2018 Rwanda iliuza nje zaidi ya kilo milioni 8.75 za matunda na kuiletea dola milioni 6.89.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |