• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soka - Ratiba ya hatua ya 16 bora ya michuano ya klabu bingwa Ulaya yatolewa

    (GMT+08:00) 2018-12-18 09:43:30

    Draw ya hatua ya 16 bora ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya imefanyika jana nchini Uswisi na kushuhudia timu tatu za Uingereza zikipangwa na timu za Ujerumani. Katika droo hiyo, wameshuhudiwa vigogo wa Bundesliga Bayern Munich wakipangwa na Liverpool ambapo Bayern itaanzia ugenini, mabingwa watetezi wa EPL Manchester City ikipangwa kuanzia ugenini dhidi ya Schalke 04 huku Burussia Dortmund pia ikipangwa na kuanza ugenini dhidi ya Tottenham Hotspurs. Manchester United imepangwa dhidi ya PSG katika hatua hiyo, ambapo itaanzia nyumbani. Michezo yote itapigwa katikati ya mwezi Februari mwakani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako