Michuano ya mabingwa wa taifa ya mpira wa mikono (handball) mwaka 2019, yanatarajiwa kutimua vumbi Januari 26. Kulingana na katibu mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Mikono la Rwanda Jean Paul Ngarambe, michuano ya wanaume itashirikisha timu 12 huku wanawake yakiwa na timu 10. Police handball ndio mabingwa watetezi kwa upande wa wanaume na Kirambo kwa upande wa wanawake. Ligi hiyo itachezwa katika mihula miwili nyumbani na ugenini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |