Leo saa mbili usiku utashuhudiwa mpambano wa kukata na shoka wakati mabingwa Patriots na mahasimu wao wakubwa Rwanda Energy Group (REG) watakapokwaana kwenye ligi ya taifa ya Kikapu nchini Rwanda katika uwanja wa Amahoro. REG na Patriots ni timu mbili pekee ambazo haziwajahi kushindwa katika msimu huu wakati ambapo REG imejikusanyia pointi 10 kutoka kwenye mechi tano iliyocheza huku Patriots ikiwa na pointi 8 na ikisaliwa na mechi moja mkononi. Msimu uliopita, Patriots iliipa wakati mgumu REG na kushinda taji la ligi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |