• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wanajeshi zaidi ya 150 wa Russia waondoka Syria

    (GMT+08:00) 2018-12-24 18:29:58

    Ofisi ya habari ya jeshi la Russia imesema, wanajeshi zaidi ya 150 wamerudi kutoka nchini Syria hadi makao makuu ya jeshi hilo ya Novosibirsk, Russia baada ya kumaliza kazi zao nchini humo.

    Taarifa iliyotolewa na ofisi hiyo imesema, katika miezi mitatu iliyopita, wanajeshi hao wa kikosi cha kukinga makombora walipelekwa kulinda usalama wa kambi ya kijeshi ya Russia nchini Syria.

    Habari zinasema, tangu mwazoni mwa mwaka huu, Jeshi la kukinga makombora la Russia limezuia mashambulizi mengi ya ndege zisizo na rubani dhidi ya kambi hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako