Ubalozi wa nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) katika mji mkuu wa Syria, Damascus umefunguliwa tena leo kwa mara ya kwanza baada ya miaka saba.
Katika taarifa yake ya hivi karibuni, naibu waziri wa mambo ya nje wa Syria amesema Syria inakaribisha hatua thabiti ya kurudi kwa balozi zote za nchi za kiarabu.
Serikali za nchi za kiarabu zilifunga balozi zake katika mji wa Damascus baada ya machafuko yaliyotokea Syria mwaka 2011.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |