Mkurungezi mkuu wa shirika hilo Yvonne Manzi Makolo amesema wataanza safari hizo mwezi Aprili mwaka ujao kwa kutumia ndege aina ya CRJ-900N.
Amesema Addis Ababa ni mji muhimu kwani ndio makao makuu ya Umoija wa Afrika na pia tume ya kiuchumi ya umoja wa mataifa kuhusu Afrika.
Sasa Rwandaair inafikisha 27 maeneo inakohudumu, Afrika Ulaya, Asia, Afrika na Mashariki ya kati.
Mwaka ujao pia shirika hilo linpanga kuanza safari za kwenda mjini, Guangzhou China, Tel Aviv, Bamako na Conakry.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |