Idadi ya watalii kutoka nje kwenda Tanzania inatarajia kuongezeka katika ukanda wa kusini baada ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) kukubali kujenga stesheni karibu na Pori la Akiba la Selous na kutenga mabehewa maalumu kwa ajili ya kupeleka watalii katika stesheni ambayo ipo karibu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Jaji mstaafu Thomas Mihayo, alisema kuwa Bodi ya Utalii ilitoa ombi hilo mwaka jana wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Tazara.
Amesema watalii wengi wanapenda sana kutembelea Selous, lakini changamoto ni namna ya kufika kutokana na ukosefu wa usafiri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |