Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Lu Kang leo amesema, makamu wa rais wa China Bw. Wang Qishan atafanya ziara nchini Uswisi kuanzia tarehe 21 hadi tarehe 24 mwezi huu, na kuhudhuria mkutano wa mwaka 2019 wa baraza la uchumi duniani la Davos.
Bw. Lu Kang amesema, kwenye mkutano huo, Bw. Wang Qishan ataeleza maoni na utetezi wa China kuhusu maendeleo ya nchi hiyo, utandawazi wa uchumi duniani na masuala mengine makuu ya kimataifa. Amesema China inakaribisha ushirikiano na pande mbalimbali kutoa mchango kwa ajili ya kujenga uchumi wa dunia wa wazi, na kuhimiza maendeleo ya pamoja ya binadamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |