Rais wa shirikisho la soka la Kenya (FKF) Nick Mwendwa amethibitisha kuwa timu ya taifa ya Kenya (Harambee Stars) itapiga kambi ya mazoezi nchini Ufaransa kujiandaa kwa michuano ya kombe la Afrika (AFCON 2019).
Akizungumza jana baada ya shirikisho la soka barani Afrika (CAF) kutangaza Misri kuandaa udamvuudamvu wa michuano hiyo katikatia yam waka huu, Mwenda amesema kambi hiyo itakuwepo kama ilivyopabgwa awali.
Kambi ya Stars nchini Ufaransa ilikuwa kwenye mizani ikitegemea mwenyeji wa AFCON 2019. Katika kikao cha awali na wanahabari, Mwendwa alifichua kwamba Kenya ingeondoa kambi yake kutoka Ufaransa kama dimba la AFCON lingepelekwa Afrika Kusini kutokana na tofauti ya majira ya mwaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |