Miaka mitatu iliyopita kampuni hizo zilikuwa zikinunua kwenye vyama hivyo kilo milioni 16, lakini katika msimu huu wa mavuno kampuni hizo zimenunua kilo milioni sita tu.
Akizungumza na wadau wa kilimo mkoani humo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mathew Mtigumwe, alisema kutokana na hali ilivyo, serikali imeamua kutafuta masoko mengine ya zao hilo.
Alisema wizara imeiagiza Bodi ya Tumbaku iende moja kwa moja kwenye nchi ambazo zinatumia sana tumbaku ili kutafuta soko la tumbaku lengo likiwa kuwasaidia wakulima.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |