• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu saba wafariki katika ajali ya ndege kaskazini mwa Iran

    (GMT+08:00) 2019-01-14 16:56:46

    Watu saba wamefariki leo baada ya ndege aina ya Boeing 707 kuanguka katika mji wa Karaj, kaskazini mwa Iran.

    Shirika la Habari la ISNA limemnukuu mkuu wa kituo cha dharura cha Iran Pir Hossein Kolivand akisema, ndege hiyo ya mizigo iliyokuwa na watu 16 ndani ilianguka kwenye eneo la makazi, kilomita 45 kutoka mji mkuu wa Tehran.

    Taarifa iliyotolewa na idara ya uhusiano wa umma ya jeshi la Iran imesema, ndege hiyo, mali ya Kyrygyzstan, ilitokea mji mkuu wa nchi hiyo, Bishkek, na ilikuwa imebeba shehena ya nyama kupeleka Iran.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako