Takwimu zilizotolewa na Idara Kuu ya Forodha ya China zimeonyesha kuwa, mwaka 2018 kampuni binafsi za China zimechangia asilimia 50 katika ongezeko la uuzaji na uagizaji wa bidhaa nje ya China, na kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya biashara ya nje.
Aidha takwimu hizo zimeonyesha kuwa, thamani ya biashara ya kuagiza na kuuza nje iliyofanywa na kampuni binafsi za China imefikia dola za kimarekani trilioni 1.79, ambalo ni ongezeko la asilimia 12.9.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |