Kampuni ya bidhaa za maabara za kimatibabu ya Lancet imetangaza mungano na ile Cerba HealthCare ya Ufaransa na kuunda kampuni mpya kwa jina Cerba Lancet Africa.
Lancet inahudumu katika nchi 14 za Afrika.
Mkurungezi mkuu wa Lancet Afrika Mashariki Dtk. Ahmed Kalebi, amesema muungano huo utaboresha huduma na kuongeza nchi wanakofanya oparesheni.
Chini ya muungano huo mpya sasa wataendesha zaidi ya maabara 100 na kuajiri zaidi ya watu 1,400.
Aidha muungano huo unaifanya Cerba Lancet Africa, kuwa mojawepo wa kampuni kubwa zaidi barani Afrika za kutoa huduma za maabara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |