Mlinzi wa timu ya Celtics Kyrie Irving hakuweza kustahimili hasira zake kwa umauzi wa mchezaji mwenzake Gordon Hayward kwa kushindwa kufunga na badala yake alilekea kwenye kona na kumpasia mchezaji mwingine wa timu yao Jayson Tatum na kudai kuwa kwa kufanya hivyo kumechangia timu yao kupoteza mchezo katika ligi ya kikapu ya Marekani (NBA) uliomalizika kwa Celtics kupoteza 105 -103 dhidi ya timu ya Magic.
Mara baada ya mchezo kumalizika, Irving alimfuata Hayward na kumfokea kwa kitendo chake kilichosababisha walinzi wa timu pinzani kuweza kuokoa goli kwa urahisi.