Serena ambaye ni bingwa wa mashindano hayo kwa mara ya saba, alitumia dakika 49 kumshinda mpinzani wake ambaye seti ya kwanza hakuambulia kitu.
Mjerumani huyo kwenye seti ya kwanza alijikuta akifumuliwa 6-0 na iliyofuata aliambuliwa 6-2 mchezo uliochezwa kwenye dimba la Laver. Ilimchukua dakika 19 tu Serena kupata pointi tano. Serena sasa anasubiri mshindi wa mechi kati ya Euginie Bouchard na Shuai Peng.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |