Cameroon na Nigeria zimetafuta njia za kushirikiana katika vita dhidi ya ufisadi. Maofisa wa Tume ya Kupambana na Rushwa ya Cameroon CONAC na Tume ya Uhalifu wa Kiuchumi na Kifedha ya Nigeria EFCC walikutana mjini Yaoundé Jumatano kutunga miongozo ya ushirikiano huo. Mwenyekiti wa EFCC Dieudonne Massi Gams amesema ufisadi sio tatizo la nchi moja bali ni la nchi zote za Afrika, na anapongeza ushirikiano kati ya Cameroon na Nigeria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |