Balozi wa Russia nchini Korea Kaskazini Alexander Matsegora amesema, madai ya Marekani kuwa Russia imeiuzia Korea Kaskazini teknolojia ya makombora na ulinzi wa anga ni ya kutungwa na hayana msingi wowote.
Balozi Matsegora amesema Marekani pia inajaribu kuhalalisha sera zake zinazoyumba katika eneo la usalama wa kimataifa.
Rais Donald Trump wa Mareklani jana alizindua Tathmini ya Ulinzi wa Makombora, ambayo inajumuisha dhamira ya nchi hiyo ya kuendeleza uwezo wake wa ulinzi wa makombora.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |