Mshindano yam bio za mwaka huu za Kilimanjaro, zinakuja kivingine baada ya mkoa wa Kilimanjaro kuanzisha mpango mahsusi kwa ajili ya kuufanya kuwa mkoa wa kijani.
Maandalizi na usaili wa mashindano hayo unaendelea huku mashidano yakitarajiwa kutimua vumbi Machi 3. Mkurugenzi wa mashindano hayo John Addison amebainisha kuwa mwaka huu wameongeza kampeni ya kutumia mbio hizo kutengeneza uoto wa asili ikiwa na lengo la kupanda miti kwenye hifadhi ya mlima Kilimanjaro ili kutunza uoto wa asili.
Mashindano hayo yatakuwa ya KM 42, KM 21 na KM 5.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |