Wawakilisji kutoka serikali ya Marekani na kundi la Taliban la Afghanistan wamefanya mazungumzo mjini Doha, Qatar.
Msemaji wa kundi la Taliban Bw. Zabihullah Mujahid amethibitisha kuwa, kundi hilo limekubali kufanya mazungumzo na Marekani baada ya nchi hiyo kukubali kuacha kukalia Afghanistan na kuitumia kushambulia nchi nyingine.
Habari zinasema, mjumbe maalum wa Marekani kuhusu suala la Afghanistan BW. Zalmay Khalilzad amehudhuria mazungumzo hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |