Watu wapatao elfu 70 wameshiriki matembezi yaitwayo "Rise for Climate" katika barabara za Brussels huku mvua ikiwa inanyesha kwa ajili ya kuishinikiza serikali ya Ubelgiji na Umoja wa Ulaya, kuongeza juhudi za kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa. Shughuli hiyo ni matembezi makubwa zaidi kuhusu hali ya hewa nchini Ubelgiji. Wapangaji wa matembezi hayo wamesema binadamu wanakabiliwa na changamoto kubwa zaidi ambayo haijawahi kushuhudiwa duniani na ni lazima wanasiasa wabebe lawama na wajibu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |