Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema, zaidi ya wahamiaji 130 hawajulikani walipo baada ya meli mbili zilizobeba wahamiaji kupinduka katika pwani ya Djibouti.
Taarifa iliyotolewa na Shirika hilo imesema, meli hizo zimezama jana asubuhi, muda mfupi baada ya kuingia kwenye Bahari Nyekundu, na kuongeza kuwa, mpaka sasa wahamiaji wawili wameokolewa na miili mitatu ya wanawake na miwili ya wanaume imepatikana.
Shirika hilo limesema operesheni ya uokoaji bado inaendelea ili kupata miili ya wahamiaji ambao hawajulikani waliko.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |