• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uingereza na Umoja wa Ulaya watofautiana kuhusu suala la mpaka wa Ireland

    (GMT+08:00) 2019-01-31 08:56:23

    Waziri Mkuu wa Uingereza Bibi Theresa May na kiongozi wa chama cha Leba Bw. Jeremy Corbyn wamefanya mazungumzo ya kwanza kuhusu Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya.

    Msemaji wa Bw. Corbyn amesema pande mbili zimefanya mazungumzo mazuri kuhusu umoja wa forodha na soko la pamoja, na kusema wanaweza kufanya mazungumzo zaidi baadaye.

    Viongozi hao wamekutana wakati Umoja wa Ulaya unajiandaa na Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya bila kuwa na makubaliano kuhusu ushirikiano kati ya pande mbili. Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Ulaya Bw. Jean-Claude Junker ameuambia Umoja wa Ulaya kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa Uingereza kujitoa bila kuwa na makubaliano yoyote.

    Bw. Junker na mwakilishi wa Umoja wa Ulaya kwenye mazungumzo ya Brexit Bw. Michel Barnier wamesema kwenye bunge la Umoja wa Ulaya kuwa watakataa juhudi za Uingereza kutaka kujadili upya suala la mpaka wa Ireland.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako