Shirika la Uhamiaji la Kimataifa IOM limesema limewasafirisha kwa hiari wahamiaji haramu 116 kutoka mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya hadi Nigeria. Hii ni mara ya kwanza kwa kazi hiyo kufanyika kutoka eneo la mashariki mwa Libya, wakati IOM inatekeleza operesheni hiyo kutoka magharibi mwa Libya, ambako wahamiaji wengi haramu wanapanga kwenda Ulaya kwa kupitia bahari ya Mediterranean.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |