Baada ya kushindwa kumaliza mbio za dunia za mwaka 2015 zilizofanyika hapa jijini Beijing kutokana na kupata jeraha la goti, Kiplimo alikaa nje ya uwanja kwa muda wote huo, lakini sasa habari ya kufurahisha kwa mashabiki wa riadha wa Uganda ni kuwa, mwanariadha huyu anarejea dimbani akiwa na nguvu mpya.
Kiplimo anatarajiwa kuongoza wanariadha wa Uganda katika mashindano yanayotarajiwa kufanyika mjini Doha mapema mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |