• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jeshi la Marekani lazuia kusafirisha misaada katika wilaya ya Hajin mashariki mwa Syria

    (GMT+08:00) 2019-02-01 16:38:39

    Shirika la habari la Syria SANA limesema, jeshi la Marekani na kikosi cha SDF kinachoungwa mkono na jeshi hilo limezuia msafara wa malori ya serikali ya Syria yanayosafirisha vitu vya msaada kuingia katika wilaya ya Hajin mkoani Deir al-Zour, mashariki mwa nchi hiyo.

    Shirika hilo limesema, msafara huo uliobeba maji ya kunywa, dawa, na vifaa vya usafi ulizuiwa na kikosi cha SDF kinachoongozwa na kundi la Wakurdi na kuarifiwa kuwa jeshi la Marekani limepiga marufuku msafara huo kuingia wilayani Hajin.

    SANA limelaani kitendo hicho cha jeshi la Marekani na kikosi cha SDF, na kusema kimekiuka sheria ya kimataifa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako