Kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii na kurasa saba za magazeti ya Kenya , idara hiyo ilichapisha majina, sura na nambari za vitambulisho za washukiwa hao, huku ikiwataka watu kupiga ripoti kwa polisi wanapowaona.
Wachunguzi hao wa makosa ya jinai aidha walitoa nambari za simu ambazo watu wanaweza kuripoti kwa kupiga simu ama kutuma jumbe fupi.
Idara ya DCI aidha ilisema kuwa ilipokea amri kutoka mahakama za Kiambu na Milimani kuwakamata washukiwa hao.
Orodha hiyo vilevile ina wanawake 30, kati ya washukiwa hao 130.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |