Sergio Aguero ameiongoza timu yake ya Manchester City kutoa dozi ya kipigo cha nguvu kwa Chelsea aka the Blues ya goli 6-0 kwenye mchezo wa ligi kuu ya Uingereza (EPL) uliochezwa usiku wa kuamkia leo uwanja wa Etihad. Aguero alipiga Hat Trick katika dakika za 13, 19 na penalti dakika ya 56, mabao mengine ya Man City yalipachikwa kimiani na Raheem Sterling na Ilkay Gundogan.
Kwa ushindi huo, Man City inafikisha alama 65 katika mechi 27 ikikwea kileleni mwa ligi hiyo kwa kuizidi Liverpool kwa magoli, Chelsea inaanguka hadi nafasi ya 6.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |