Jeshi la Venezuela jana limefanya rasmi mazoezi makubwa ya kijeshi ili kuonesha nia thabiti ya kupinga uingiliaji kutoka nchi za nje.
Rais Nicholas Maduro wa Venezuela amesema, serikali yake itahakikisha imewekeza zaidi katika jeshi ili kuhakikisha mahitaji ya utaratibu wa ulinzi wa anga ya nchi hiyo.
Pia amesema, Venezuela ina haki ya amani kwani watu wa Venezuela wanapenda amani, na kwamba nchi hiyo haitakubali kutishiwa au mambo yake ya ndani kuingiliwa na mtu au nchi yoyote. Amelitaka jeshi na watu wa Venezuela kushirikiana ili kukinga mashambulizi ya Marekani dhidi ya nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |