Mradi wa kawi wa Kenya na Tanzania waanza
Mradi wa Ushirikiano wa umeme wa Kenya naTanzania umeanza huku nchi hizo zikilenga kutumia kwa pamoja kawi hasa kwenye maeneo ya mipakani.
Mradi huo umegawanywa katika maeneo kadhaa, na makandarasi upande wa Tanzania wameahidi kufanyauunganishaji wa laini za KV400 za urefu wa kilomita 510 kabla ya 2020.
Upande wa Tanzania mradi huo unatekelezwa na Kampuni ya Ugavi wa Umeme (Tanesco) kupitia mkopo wa dola milioni 258.82 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika na Shirika la Kimataifa la Ushirikiano la Japan.
Mbali na kuungana na Tanzania Kenya pia itaongeza laini zake hadi Ethiopia, nayo Tanzania hadi Zambia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |