Rais mpya wa DR Congo Felix Tshisekedi anasema nchi yake iko tayari kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ili kuimarisha uhusiano wake wa kiuchumi na kanda.
Tshisekedi alisema kuwa EAC itafaidi wananchi wa Congo zaidi, hasa wale wanaoishi katika la mashariki mwa nchi hiyo.
Akizungumza wakati alipokutana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwenye ziara yake hivi karibuni, Tshisekedi, alisema kujiunga na jumuiya hiyo kutasadia kukua kwa uchumi wa nchi yake.
Walikubaliana kuimarisha mahusiano kati ya nchi hizo mbili huku rais Kenyatta akiahidi kuwa serikali yake itasaidia kutoa mafunzo kwa watumishi wa umma wa DRC.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |