• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Makamanda wa kijeshi wa Umoja wa Afrika wajadili mpango wa kuondoa jeshi nchini Somalia

    (GMT+08:00) 2019-02-12 09:51:55

    Makamanda wa Tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM wameanza mkutano wa siku nne ili kujadili mpango kamili wa kuondoa jeshi lao nchini humo.

    Naibu mkuu wa tume hiyo Simon Mulongo amesema, mpango huo utaamua shughuli na operesheni zitakazotekelezwa chini ya dhana mpya ya CONOPS, na pia kuweka muda na kutoa uungaji mkono wa vifaa vinavyohitjika ili kutekeleza shughuli hizo.

    Mkutano huo umewaleta pamoja makamanda wa vikosi mbalimbali kutoka nchi zao wanazoziwakilisha, wawakilishi kutoka jeshi la taifa la Somalia na wajumbe wa Umoja wa Mataifa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako