• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Klabu Bingwa Afrika- Simba SC yawagonga waarabu, JS Saoura yaisimamisha AS Vita

    (GMT+08:00) 2019-02-13 09:00:51

    Katika nyakati ngumu unahitaji mashujaa watakaokuweka mgongoni na kukuvusha kuelekea kule ambako unahitaji kufika. Ndivyo unavyoweza kusema kwa wachezaji wa timu ya Simba ya Tanzania ambao kwa takribani majuma mawili wamekuwa wakibezwa na baadhi ya wadau wa soka nchini humo.

    Simba sasa imefufua matumaini ya kwenda robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya ushindi wa goli 1-0 dhidi ya timu bora Afrika Al Ahly ya Misri katika mchezo wa kundi D uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

    Alikuwa mchezaji raia wa Rwanda anayechezea klabu hiyo ya Simba Meddy Kagere ndiye aliyewanyanyua mashabiki waliofurika kushuhudia Muarabu akipigishwa kwata.

    Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, JS Saoura ya Algeria imeitwanga AS Vita ya DRC kwa bao 1-0. Kwa ushindi huo, Saoura iliyokuwa nyumbani Algeria, unafanya Simba kubaki katika nafasi ya pili, Al Ahly wakiongoza kundi hilo, huku Saoura na Vita wakiwa katika nafasi ya tatu na ya nne.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako