Wapiganaji zaidi ya 50 wa jeshi la SDF la Syria linaloungwa mkono na Marekani na kundi la Isamic State wameuawa katika mapambano ya siku nne zilizopita mashariki mwa Syria. Shirika la Uangalizi wa Haki za Binadamu la Syria limesema kwa sasa wapiganaji wa IS wamezingirwa na jeshi hilo katika eneo la kilomita mbili za mraba katika eneo la mashariki mwa mto Euphrates.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |