Taarifa hiyo ya TFF imeeleza kuwa kamati hiyo itaongozwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda atakayekuwa mwenyekiti na katibu ni Mhandisi Hersi Said.
Jukumu kubwa la kamati hiyo ni kuhakikisha timu hiyo ya taifa inapata ushindi katika mchezo wake wa mwisho wa kundi L kuwania tiketi ya AFCON dhidi ya timu ya taifa ya Uganda (Uganda Crane) mechi itakayochezwa uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam Machi 22.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |