Wadau kwenye sekta ya uchukuzi wa anga kutoka Afrika wanakutana kwa siku mbili mjini Kigali nchini Rwanda kujadili maswala ya usalama na taaluma kwenye sekta hiyo.
Mkutano huo unawaleta pampja wakuu wa mashirika ya ndege, watunga sera na watoa huduma kwenye sekta hiyo.
Miongoni mwa maswala mengine yanayojadiliwa ni pamoja na vikwazo vya ukuaji, taratibu na mapato kwenye sekta ya usafiri wa anga.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |