Simba wameifunga Stand United kwa mabao 2-0 uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Mabao ya Simba yamefungwa na John Bocco aliyefunga mabao yote mawili.
Mechi nyingine za ligi hiyo, wakata miwa wa Turiani Mtibwa imeibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Mbao FC, nayo Singida United imewashinda Wajelajela Tanzania Prisons 2-1, Kagera sugar imeisambaratisha Lipuli kwa mabao 2-0 huku Mbeya City wakilazimishwa sare ya 0-0 na Ndanda FC.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |