Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang amesema kwenye ripoti ya kazi ya serikali aliyoitoa leo kuwa, China imeweka lengo la ongezeko la Pato la Ndani GDP kwa mwaka huu kuwa ni kati ya asilimia 6 na 6.5.
Ili kutimiza lengo hilo, China itaendelea kutekeleza sera chanya za fedha, kutoa kipaumbele katika utoaji wa ajira, kuimarisha uratibu na ushirikiano kati ya sera mbalimbali, na kuhakikisha uchumi unaendelea katika kiwango mwafaka, ili kuhimiza uchumi na jamii kupata maendeleo endelevu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |