Borussia Dortmund ya Ujerumani, ilikuwa na kibarua dhidi ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza, na matokeo ni kuwa, Tottenham imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Dortmund.
Mechi ya mzunguko wa kwanza, wawakilishi hao wa Ujerumani, walifungwa mabao 3-0 ugenini.
Mchezo mwingine ulikuwa kati ya Real Madrid ya Uhispania iliyokuwa kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Bernabeu na kukubali kipigo cha maana toka kwa Ajax ya Uholanzi kwa magoli 4-1.
Usiku wa kuamkia kesho kutakuwa na michezo minne itakayopigwa baina ya FC Porto itakapovaana na AC Roma, nayo Paris Saint Germain itaumana na Manchester United.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |