Timu ya karate ya Kenya imezoa medali 39 katika mashindano ya karate ya dunia yanayofahamika kama Asian International World Funakoshi Shotokan Karate Organization (WFSKO) yaliyomalizika mwishoni mwa wikiendi mjini Mumbai, India.
Kocha wa kikosi cha timu hiyo Elizabeth Rukwaro amesema aliongoza wanakarate wapatao 32 ambao ni wenye umri kati ya miaka minne na 17 kutoka Kaunti ya Kiambu na Murang'a.
Amefahamisha kwamba, nchi nyingine zilizoshiriki ni Sri Lanka, Kyrgyatan, Malaysia, Nepal, Iran, Uingereza, Armenia, Mauritius, Bhutan, na Kenya.
Kenya imefuzu kucheza kwenye mashindano ya dunia ya Karate yatakayofanyika nchini Uingereza mwezi Novemba mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |