• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • UNHCR yaunga mkono wakimbizi kurudi nyumbani kwa hiari na usalama

    (GMT+08:00) 2019-03-10 18:12:50
    Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) Bw. Filippo Grandi amesema kwamba shirika hilo litaendelea kutoa msaada kwa wakimbizi wa Syria nchini Lebanon ili kuunga mkono kurudi nyumbani kwao kwa hiari na usalama.

    Bw. Grandi ambaye yuko ziarani huko Beirut nchini Lebanon amesema kwa mujibu wa uchunguzi wa UNHCR, wakimbizi wengi wa Syria nchini Lebanon wanapenda kurudi nyumbani kwao, ingawa wana wasiwasi juu ya masuala ya usalama wa Syria, makazi, na mahitaji ya kimsingi ya maisha, pamoja na masuala mengine ya kisheria.

    Hata hivyo Bw. Grandi amesema kuwa UNHCR inashirikiana na serikali ya Syria kutatua masuala hayo.

    Kutokana na makadirio ya serikali ya Lebanon, Wasyria wapatao milioni 1.5 walikimbia Lebanon toka msukosuko wa Syria kulipuka waka 2011.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako