• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda: Wanawake Uganda wapanga kuanza kituo cha biashara

    (GMT+08:00) 2019-03-12 19:17:42
    Kundi la wanawake wajasiriamali nchini Uganda wanatafuta shilingi bilioni 20 ili kuanzisha kituo cha biashara katika wilaya ya Mukono.

    Kituo hicho kitakuwa na huduma kama vile mabohari na uongezaji wa ubora kwenye bidhaa.

    Aidha kitakuwa na maabara, taasisi ya mafunzo na huduma za kisheria kwa wanawake.

    Mwenyekiti wa chama cha wanawake wafanyabishara nchini humo Angela Bageine, amesema kituo hicho kitasaidia wanawake kujinufaisha na fursa za kibiashara na kujikuza kiuchumi.

    Fedha hizo zitatoka kwa michango ya wanachama na washirika wengine wanaounga mkono wanawake.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako