• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Viwanda vya maziwa Tanzania vyakosa maziwa

    (GMT+08:00) 2019-03-12 19:19:07
    Kampuni ya usindikaji wa maziwa ya Tanga Fresh nchini Tanzania, imetaja sababu za wafugaji wengi kushindwa kuzalisha maziwa yanayokidhi viwango ikiwamo kuchanganya maji kwenye maziwa.

    Meneja Mkuu wa Tanga Fresh, Michael Karata alisema kiwanda hicho kinahitaji lita 120,000 kwa siku lakini mpaka sasa wanasindika lita 50,000 tu.

    Alisema, sehemu kubwa ya maziwa wanategemea kutoka kwa wafugaji lakini wameshindwa wameshindwa kukidhi mahitaji ya kiwanda.

    Licha ya kuchanganya maziwa na maji, Karata alisema sababu nyingine ni ng'ombe kukosa lishe bora na ukame.

    Alisema awali walilazimika kununua maziwa nje ya nchi, lakini kwa sasa hawafanyi hivyo na kwamba licha ya kuongeza vituo vya kukusanyia maziwa kwa baadhi ya mikoa, bado kiasi kinachopatikana hakikidhi mahitaji ya kiwanda.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako