Kwenye dili hilo la mwaka mmoja lililosainiwa jana, kampuni ya kubeti ya Betin imeingia mkataba huo wa shilingi milioni 20 na shirikisho la soka la Kenya (FKF), dili ambayo itagharamia maandalizi ya timu hiyo, gharama ya jezi za timu na za mashabiki.
Akizungumza mara baada ya kusaini makubaliano hayo, rais wa FKF Nick Mwendwa amesema udhamini huo utasaidia kuwezesha kambi ya Harambee Stars ambayo imepangwa kuwa nchini Ufaransa wiki tatu kabla ya kuelekea Misri.
Harambee stars inayoongoza kundi D itaondoka nchini Kenya Machi 22 kuelekea jijini Kumasi Ghana kwa ajili ya mechi ya mwisho ya kundi hilo kufuzu AFCON.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |