Macharia amesema CRBC ni kampuni ambayo imeonyesha uwezo wake na ana imani kuwa itafanya kazi nzuri. Serikali tayari imeagiza injini za treni za dizeli kwa gharama ya shilingi bilioni 1.5 kutoka nchini Huispania. Injini hizo zitaunganishiwa mabehewa na kuanza kutoa huduma za usafiri kwa wenyeji wa jiji la Nairobi na viunga vyake. Reli ya sasa imezeeka na ina kasi ya chini ya kilomita 15 kwa saa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |