Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Lu Kang amesisitiza kuwa wizara hiyo na ubalozi wa China nchini Ethiopia zitafuatilia utaratibu wa kurejesha miili ya raia wanane wa China waliofariki katika ajali ya ndege ya Ethiopia, na kuratibu idara husika kutoa misaada kwa familia za marehemu hao.
Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia iliyokuwa na watu 157 ilianguka jumapili iliyopita, na kusababisha vifo vya watu wote walioko ndege hiyo wakiwemo raia 8 wa China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |