Maseneta nchini Marekani wamefanikiwa kuzuia jaribio la rais Donald Trump kutangaza hali ya dharura kwenye mpaka wa kusini kwa kura 59 dhidi ya 41. Hatua hiyo iliyoambatana na kura zilizopigwa na baraza la wawakilishi, inatarajiwa kumlazimisha Rais Trump kutumia haki yake ya turufu kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani. Hii pia ni mara ya kwanza kwa bunge kukataa azimio la hali ya dharura ya taifa tangu Sheria ya Dharura ya Taifa ianze kutekelezwa mwaka 1976.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |